Saturday, May 12, 2012

Airtel Yatoa Msaada wa Madawati na Mipira kwa shule za Msingi za Maarifa, Mwangaza na JICA zilizopo Gongolamboto Jijini Dar

Mchezaji wa zamani wa Klabu ya Manchester United ya Uingereza Quinton Fortune, akikabidhi moja ya madawati yaliyotolewa na Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel kwa Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi ya Maarifa Mareitha Mulyalya huku Naibu Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Elimu), Mh Kassim Majaliwa akitazama. Kampuni ya Airtel Tanzania ilitoa mipira 30, jesi seti tatu na madawati 40 kwa shule za msingi za Maarifa, JICA na Mwangaza zote za Gongo La Mboto, Dar es Salaam.
Mchezaji wa zamani wa Manchester United ya Uingereza Quinton Fortunewa pili kulia, akionyesha waandishi wa habari (hawako pichani) baadhi ya vifaa vya michezo vitakavyotumika kwenye michuano ya soka ya kimataifa kwa vijana wenye umri chini ya miaka 17 ya Airtel Rising Stars jana kwenye Hoteli ya Sea Cliff jijini Dar es Salaam. Kati ni Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Technologia Mh. Professa Makame Mbarawa, wa kwanza kulia ni Mkurugenzi Mashindano wa TFF Sandy Kawembe, Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Tanzania Sam Elangallor na Mkurugenzi Bidhaa Airtel Afrika Obina Justine.
Mchezaji wa zamani wa Klabu ya Manchester United ya Uingereza Quinton Fortune, akipiga mpira kuashiria uzinduzi rasmi wa michuano ya vijana wenye umri chini ya miaka 17 ya Airtel Rising Stars. Uzinduzi huo ulifanyika jana, Mei 10, kwenye Hoteli ya Sea Clif, jijini Dar es Salaam.
Msanii wa kizazi kipya Ambwene Yesaya maarufu kama AY, akiwatumbuiza wanafunzi wa Shule ya Msingi ya Maarifa iliyopo Gongo La Mboto nje kidogo Jijini Dar es Salaam wakati Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel ilipotoa msaada wa madawati 30, mipira ya miguu 40 na jezi seti tatu, Alhamisi Mei 10, 2012 ambapo mgeni rasmi alikuwa Naibu Waziri kwenye Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mtaa (Elimu) Mh. Kassim Majaliwa. Shule zingine zilizofaindika na msaada ni Maarifa, JICA na Mwangaza zote za Gongo La Mboto, Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment