Monday, May 21, 2012

FINALI ZA KOMBE LA MAGIC SITE -IRINGA

ZAWADI YA KOMBE
KAPTENI WA TIMU YA MASHINE TATU AKIPOKEA KOMBE LA MSHINDI WA KWANZA
KAPTENI WA TIMU YA VIZIWI AKIPOKEA ZAWADI
KAPTENI WA TIMU YA ZIZI LA NGO'MBE AKIPOKEA KOMBE LA MSHINDI WA PILI
MDHAMINI WA MASHINDANO YA MKWAWA MAGIC SITE NGD STEVEN NYANDONGO
 
Hitimisho la mashindano yaliyokuwa yakiendeshwa  katika Manispaa ya Iringa  yamemalizika leo. Mashindano hayo yalijumuisha timu katika mitaa yote ya Manispaa ya Iringa. Akieleza mdhamini wa mashindano hayo  Ndg. Steven Nyandongo  Mkurugenzi wa kituo cha Utalii Mkwawa Magic Site alisema  nia ya mashindano hayo ni kuwapa changamoto vijana katika mchezo wa mpira wa miguu na kuwafanya  wajitume kimazoezi zaidi ili  hapo baadaye tuweze kupata  wachezaji  watakaosababisha Ligi Kuu ichezwe hapa kwetu Iringa.

Akielezea gharama za ujumla katika michezo hiyo ni shilingi milioni tatu ambazo zimegawanywa  kwa matumizi yafuatayo:
§  Posho kwa Waamuzi
§  Viburudisho kama vile maji, soda n.k
§  Zawadi kwa timu zote zilizoshiriki mashindano haya na kila timu ilipata mpira mmoja mmoja.

Zawadi  ya mfungaji bora aliyepata seti ya viatu vya mpira kutoka Timu ya Viziwi ya Mtwivila.
Zawadi kwa Golikipa bora aliyepata seti ya jezi moja.
Ngao kwa timu yenye nidhamu ilichukuliwa na Timu ya Viziwi ya Mtwivila
Zawadi kwa washindi wa pili ambao walipata Kikombe, mpira na mbuzi mmoja Timu ya Zizi la Ng’ombe
Zawadi kwa mshindi wa kwanza aliyepata Kikombe, mpira, seti ya jezi  pamoja na mbuzi mmoja nao ni Timu ya Mashine tatu.

Akitoa shukrani Katibu wa Chama cha mpira wa miguu Iringa Ndg. Eliud Mvela  aliomba mashindano haya yawe yanafanyika kila mwaka na wao kama chama watashiriki kusaidia namna  ya uendeshaji.

No comments:

Post a Comment