Wednesday, May 23, 2012

WIKI HII CHUO KIKUU TEOFILO KISANJI (TEKU)

KAMPENI ZA UCHAGUZI CHUO KIKUU CHA TEOFILO KISANJI (TEKU) ZAZINDULIWA RASMI.

*Wanawake wawili wajitokeza kugombea nafasi ya Urais na Makamu Rais.
Kampeni za uchaguzi wa kumpata Rais wa Chuo kikuu cha Teku, zimezinduliwa rasmi jana katika ukumbi wa Mwasakafyuka huku wagombea wakinadi sera zao.

Kampeni hizo zilizinduliwa na Dakta Mozes D, na kusimamiwa na mkufunzi wa chuo Bwana Alawi Mikidadi ambapo Mkurugenzi wa uchaguzi Bi Nyemba Joyce aliweka hadharani wagombea watakao wania viti vya urais na makamu rais.

Majina hayo upande wa rais ni Bi Somi Irene, Bwana George Godbless na Joshua Jason na upande wa Makamu ni Bi Wilson Gwantwa, Bwana Yohanna Yesse na Deus Petro.

Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi Bwana Kavenga Emmanuel amesema kwamba mchakato wa uchaguzi ulianza Mei 9 mwaka ahuu kwa kujaza fomu ambapo wanachuo 70 walijitokeza kuomba nafasi mbalimbali.

Aidha Mei 19 na 20 wagombea walifanyiwa wagombea usaili na kwamba majina yaliyotajwa hapo juu ndio yaliyopitishwa na tume hiyo na kwamba kampeni zimeanza rasmi jana ambazo zitaendelea mpaka Mei 28 asubuhi na uchaguzi utafanyika Mei 29 mwaka huu na matokeo yatatangazwa mei 30 mwaka huu na viongozi wote Rais na baraza la mawaziri kuapishwa Juni mosi mwaka huu.

Mwenyekiti huyo Bwana Kavenga amewataka viongozi hao kufanya kampeni za amani bila matusi kwani kampeni kwa kufanya hivyo haitawasaidia kupata kura, bali itawashushua heshima zao.

Kwa upande wake Rais anayemaliza muda wake Bwana Ambukege Imani ameishukuru tume ya uchaguzi kwa mchakato mzima na anafurahi kumaliza muda wake chuo kikiwa na amani na kuwataka watakaopata nafasi za kuongoza wazingatie sheria, demokrasia na upendo ili kuleta mshikamano katika chuo, ili wanaoongozwa wajisikie kuwa na amani kuwepo chuoni hapo badala ya kutatua migogoro isiyokuwa na maana.

Baadhi ya wabunge walipita bila kupingwa, kutokana na baadhi ya maeneo waliyokuwa wakiyagombea kutokuwa na wapinzani.

Hata hivyo kujitokeza kwa wanawake kumeleta msisimko wa uchaguzi huo huku wanawake wakitoa majigambo kuwa wanawake wanaweza hata pasipo kuwezeshwa na kwamba chuo hicho hakijawahi kupata viongozi wa juu ambao ni wanawake na kwamba imefika zamu yao kuongoza.
Habari na Ezekiel Kamanga. 

No comments:

Post a Comment