Thursday, May 31, 2012

MISS UNIVERSE TANZANIA 2011/2012 KESHO KUONGOZA HARAMBEE YA KUCHANGIA MFUKO WA SARATANI YA MATITI TANZANIA .


Na.Mwandishi wetu
Mrembo anayeshikilia taji la Miss Universe Tanzania 2011/2012 Nelly Kamwelu kwa kushirikiana na Mfuko wa Saratani ya Matiti Tanzania (Breast Cancer Foundation) leo atafanya harambee ya kuchangia mfuko wa saratani ya matiti itakayofanyika kwenye Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
Harambee hiyo imepangwa kuanza saa 1.00 usiku kwa mujibu wa muandaaji wa mashindano ya Miss Universe Tanzania na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Compass Commutations, Maria Sarungi Tsehai.
Maria alisema kuwa katika hafla hiyo kutakuwa na mnada wa kito cha Tanzanite ambayo imetolewa maalum na  kampuni ya Richland Resources kwa ajili ya kuchangia mfuko huu. Pia picha ya Mrembo wa Miss Universe Tanzania itanadiwa katika mnada huo.
Mrembo Nelly Kamwelu toka achukue taji la Miss Universe Tanzania 2011, amekuwa akifanya kazi bega kwa bega na mfuko wa saratani ya matiti ikiwamo kusaidia kutoa elimu katika shule mbalimbali ili kupunguza au kutokomeza uwezekano wa kuenea kwa saratani ya matiti. Mfuko huu umepanga kuendeleza elimu hii kwa shule za mikoa ya Mbeya, Ruvuma, Rukwa, Iringa, Mtwara na Lindi.
Kwa kusindikiza hafla hii kutakuwa na maonyesho ya mavazi yaliyotolewa na wabunifu wa hapahapa nchini ambao ni Escado Bird, Kemi Kalikawe na Subira Wahure vilevile kutakuwa na burudani ya muziki kutoka msanii Enika na mchekeshaji Evans Bukuku. Pia mrembo mwenyewe Nelly Kamwelu atatoa burudani ya dansi aina ya Belly Dance.

No comments:

Post a Comment