Thursday, May 10, 2012

SERIKALI YA INDIA KUTOA ZAWADI NONO 18 KWA VIJANA KUTOKA AFRIKA NA INDIA KUPITIA MPANGO WA “INDIAFRICA”


Mkurugenzi wa Project ya Indiafrica Dr. Seema Kundra akifafanua mchakato mzima wa Indiafrica ( A Shared Future) utakavyokuwa nchini Tanzania.

Mwakilishi kutoka Ubalozi wa India Kunal Roy (wa kwanza kulia) akielezea sababu za Ushiriki wa Serikali ya India katika Project ya Indiafrica.

Mbunifu wa Mavazi kutoka Tanzania Mustafa Hassanali (kushoto) akifafanua ushiriki wa vijana wadogo wanaochipukia katika nyanja za ubunifu na jinsi watakavyofaidika kupitia ushirikiano wa Swahili Fashion Week na Indiafrica.

Mwakilishi kutoka chuo Kikuu cha Dar es Salaam Dr. Mbura akizungumza jinsi mdahalo kuhusu Indiafrica utakavyoendeshwa katika Ukumbi wa Nkurumah Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
INDIAFRICA (A Shared Future) ni mpango wa kimawasiliano unaojumuisha mashindano mbalimbali kama, uandishi wa insha, upigaji picha na ubunifu. Hii itasaidia kujenga jukwaa la vijana kutoka Afrika naIndiawenye vipaji na uwezo wa kushirikiana katika changamoto na mafanikioyao; Na baadae kushirikiana kiubunifu, biashara na utamaduni.
Kwa Tanzania mchakato mzima itakuwa tarehe 12 Mei 2012 ukumbi wa Nkuruma chuo kikuu cha Dar-es-salaam kuanzia saa 2:00 asb-7:00mch awamu ya pili itakuwa saa 8:00-11:00jioni.
Baada ya mdahalo jioni wasanii Chid Benzi na Dully Sykes kutoka Tanzania watatoa burudani kwa washiriki vijana wajasiliamali wenye maono ya mafanikio na maendeleo. Washindi watapata fursa ya kutembelea Afrika na India.

No comments:

Post a Comment