Saturday, June 30, 2012

WANAHARAKATI WALIPOKUWA WANAMUAGA DR, ULIMBOKA KWENDA NG'AMBO KWA MATIBABU ZAIDI

 Wanaharakati leo walipomuaga Dkt. Ulimboka kwenda n'gambo Ni katika Uwanja wa Ndege wa Kimtaifa wa Mwalimu Julius Nyerere, Dar es Salaam wakati wa  kumsindikiza Dkt. Ulimboka  kwenda ng'ambo kwa ajili ya  vipimo vya ziada na matibabu  stahiki baada ya majibu ya vipimo  hivyo ambavyo imeshindikana kuvipata nchini kutokana na ama kuharibika kwa vifaa hivyo au kukosekana kabisa.
Mabango ya Madaktari,
 Umma hauna budi kutambua kuwa bila ya vipimo sahihi, ni  vigumu sana kutoa matibabu sahihi. Wagonjwa wengi  wamepoteza uhai kutokana na kukosekana vipimo kwa ajili ya  kufanya uchunguzi mbalimbali
 kabla ya kufikia uamuzi  "diagnosis" kwa ajili ya matibabu  sahihi, na hivyo Madakari  wamebaki wakitumia zaidi uzoefu wao.
 Hili ni mojawapo ya mambo  ambayo Madaktari wamekuwa  wakijitahidi kulieleza na kutaka  lifanyiwe kazi na Serikali, ili  waweze kutumia vyema kisomo  chao na kukuza uwezo wao wa  kutafiti na kutibu magonjwa  mbalimbali. Kukosekana kwa vifaa ndiyo moja ya mambo makubwa
 kabisa yanayochangia wagonjwa  wanapelekwa nje ya nchi. Ukweli wa usemi huu unadhihirika pale Madaktari wa  Kitanzania wanapohamia nchi za  ng'ambo na kufanya kazi katika  nchi hizo kwa ufanisi. Ikiwa Madaktari hawa wasingekuwa na  uwezo na maarifa, haiyumkini  wasingeweza kufanya kazi huko waendako.
 Dkt. Ulimboka ameondoka akiwa  chini ya ulinzi mkali wa Madaktari  huku wanaharakati, baadhi ya  madaktari na wananchi  wakereketwa wakionesha  mabango ya kulaani unyama aliofanyiwa Dkt. Ulimboka
 Source:wavuti.com

No comments:

Post a Comment