Sunday, June 3, 2012

KAMPENI ZA UCHAGUZI WA SERIKALI YA WANAFUNZI UDOM WAKOSA MVUTO

KAMPENI ZA UCHAGUZI WA NAFASI MBALIMBALI ZA UONGOZI UDOM WAKOSA MVUTO,WANAFUNZI HAWATAKI SIASA

Mmoja wa Wanafunzi wa Chuo Kikuu Cha Dodoma (UDOM) akinadi Sera zake kwa wanafunzi wenzake na kuomba kura kwaajili ya wanafunzi kuweza kumchagua ili awe mbunge kutoka katika Kitivo Cha sayansi ya Jamii.
Mwanafunzi mwingine naye aliweza kuomba kura kwa baadhi ya wanafunzi ambao walihudhuria kampeni zake katika kampeni zinazoendelea tayari kwa uchaguzi wa serikali ya wanafunzi unaotarajiwa kufanyika june 2012
Hiyo Ndio kambi moja wapo katika kampeni za kuwania nafasi mbalimbali katika serikali ya wanafunzi wa UDOM wakiwa katika kampeni huku wengine wakisubiri kupiga  kampeni kitu ambacho wanafunzi wengi wamepuuzia na kudharau kampeni.
Wanafunzi Wachache waliojitokeza kusikiliza kampeni za wagombea wa nafasi mbalimbali za uongozi katika serikali ya wanafunzi UDOM
Meneja Kampeni akiwapigia Debe wagombea wake huku wanafunzi wengi  wakiwa hawana habari na kampeni na kuendelea na mambo yao kama wanavyoonekana pichani

Kuonyesha kwamba Siasa pamoja na Kampeni zimekosa mvuto wakati wagombea wakinadi sera zao hao huku wao wakitaniana kuhusiana na uchaguzi wa serikali ya wanafunzi hutakavyokuwa na mwamko mdogo huku wengine wakisema hawatapiga kura kabisa kabisa
Hili ndio kundi la watu waliohudhuria kampeni za wagombea wa nafasi mbalimbali katika serikali ya wanafunzi UDOM.

No comments:

Post a Comment