Sunday, October 21, 2012

MISS EAST AFRICA 2012 TANZANIA YATANGAZA MREMBO WAKE


 
Mrembo atakaewakilisha Tanzania katika mashindano ya mwaka huu ya Miss East Africa ni JOCELYNE DIANA MARO (22)

 Mrembo huyo alipatikana kufuatia mchakato ulioendeshwa na kamati maalum ya kuratibu zoezi hilo kwa zaidi ya miezi mitatu iliyopita na kuwashinda warembo wengine 148  waliojitokeza kutaka kuiwakilisha Tanzania katika mashindano ya Miss East Africa 2012
 Jocelyne amehitimu shahada ya Business Economics mwezi wa saba mwaka huu katika chuo kikuu cha Keele University, Nchini Uingereza

 Maandalizi ya mashindano hayo yanaendelea vizuri na yapo kwenye hatua za mwisho ikiwa ni pamoja na kukamilisha taratibu zote za BASATA ili kufanikisha mashindano hayo yatakayofanyika tarehe 07 December, 2012 katika ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es salaam

 Mashindano ya Miss East Africa mwaka huu tayari yameanza kuvuta hisia za watu wengi barani Africa kufuatia kiwango cha juu cha warembo wanaowania taji hilo.

 Nchi zilizothibitisha kushiriki mashindano hayo ni wenyeji Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi. Nchi zingine zilizoalikwa kushiriki ni pamoja na Ethiopia, Eritrea, Somalia, Djibouti, Southern Sudan, Malawi, pamoja na visiwa vya Seychelles, Madagascar, Reunion, Comoros, na Mauritius.

 Mashindano ya Miss East Africa yanalenga kukuza ushirikiano na kutangaza utamaduni wa Afrika Mashariki, pamoja na kutangaza utalii wa Tanzania kama Nchi wenyeji wa mashindano hayo makubwa katika ukanda huu wa Afrika

 Mashindano ya Miss East Africa yanamilikiwa na kuandaliwa na kampuni ya Rena Events Ltd ya jijini Dar es salaam,.

No comments:

Post a Comment