Thursday, November 15, 2012

WANAFUNZI WA KITANZANIA WANA KUFAA NJAA HUKO URUSI,,,,!! WA HUSIKA SAIDIENI HAWA WATOTO,,,,,!!!

Sisi wanafunzi wa kitanzania nchini Urusi ,tunakosa huduma za msingi kama vile malazi , chakula na bima ya afya.

Serikali kupitia bodi ya mikopo ya elimu ya juu na Wizara ya Elimu na mafunzo ya ufundi ,kwania njema iliamua kusomesha wanafunzi wa kitanzania katika nchi mbalimbali duniani ikiwemo Urusi.
Lakini kutokana na utendaji mbovu na ubinafsi wa baadhi ya watendaji wa Bodi ya mikopo, kumekua na ucheleweshwaji wa ulipaji wa pesa za kujikimu , malazi na bima ya afya kwa zaidi ya miezi mitatu sasa bila sababu za msingi toka kuanza kwa mwaka wa masomo 2012/13.

Hali hii imetupelekea wanafunzi kuanza kufukuzwa katika hosteli tunazoishi pamoja na kutopatiwa huduma za afya pindi tunapo ugua.Ikumbukwe kuwa katika nchi za ulaya huwezi pata matibabu kama huna bima ya afya.

Shukrani zetu za dhati ziende kwa Ubalozi wa Tanzania nchi Urusi kwa kushirikiana bega kwa bega na Wanafunzi katika kutafuta ufumbuzi wa tatizo hili linalotukabili katika kipindi hiki kigumu pamoja na majuku mengi waliyonayo, pamoja na jitihada hizo mpaka sasa hakuna ufumbuzi wowote uliopatikana.

Tunaandika waraka huu kwa huzuni na masikitiko makubwa sana kwa sababu kutopatiwa mikopo mpaka sasa sio tu kunafanya wanafunzi waishi maisha magumu na hatari, vilevile kunatia aibu Taifa kwa kutolipa ada kwa wakati.

Tunaamini kabisa Serikali kupitia bodi ya mikopo ,wizara ya elimu na mafunzo stadi na ufundi na ubalozi wa Tanzania Nchini Urusi una nia njema kabisa kusomesha vijana wake nje ya nchi, ispokua tu kuna baadhi ya watendaji wa bodi ya mikopo wamekua wazembe na kutowajibika kwani wamekua wakitoa majibu ya uongo na jeuri kwa uongozi wa wanafunzi na maafisa wa ubalozi wa Tanzania nchini Urusi.

Ombi letu kwenu ni kutufikishia ujumbe huu kwa wahusika na watendaji wa ngazi za juu za bodi ili waweze kutusaidia sisi wanafunzi wa Urusi ambao tupo hatarini huku ugenini.

Tunatumaini kutokana na Uzito wa tatizo letu wahusika watalishughurikia na kulitatua tatizo hili kwa haraka zaidi na kutupa ufafanuzi wa ucheleweshwaji wa mikopo ya wanafunzi kwa zaidi ya miezi mitatu(3).
WANAFUNZI NCHINI URUSI.

6 comments:

  1. I like it when folkѕ come togethег and
    ѕhare ideas. Grеat blog, κeeρ it up!
    Also visit my web page - webstarts.com

    ReplyDelete
  2. Whoa! This blog looks just like my old one! It's on a totally different subject but it has pretty much the same page layout and design. Outstanding choice of colors!

    My blog post endurosmale.net

    ReplyDelete
  3. Howdy! This post couldn't be written any better! Reading through this post reminds me of my good old room mate! He always kept talking about this. I will forward this page to him. Fairly certain he will have a good read. Thanks for sharing!

    my website ... online airplane games

    ReplyDelete
  4. Everyone loves what you guys are up too. This kind of clever work
    and exposure! Keep up the terrific works guys I've incorporated you guys to my own blogroll.

    Feel free to visit my weblog :: 8:43 AM

    ReplyDelete
  5. you are in гeality а good ωеbmasteг.
    The site loading speed іs incredible. It kind of feels that уοu аre dоing anу uniquе trick.
    Alsο, The cоntents агe mаѕterwοrκ.

    you hаve рerfoгmed а fantastic
    prοcеsѕ in this ѕubjеct!


    Heгe is my web page: buy hcg injections

    ReplyDelete
  6. My family memberѕ evеry timе say thаt I am wastіng mу timе here at net, except I knοw I
    am gеtting familiаrity ԁaily by reading thes fаstidіouѕ articles.


    Feel free tο ѵisit mу homepage:
    dieta hcg
    my web site :: pure hcg

    ReplyDelete